Baada
ya wapenzi wa muziki Tanzania kusubiri kwa muda mrefu sasa wamepata
nafasi ya kujiburudisha na ngoma mpya kutoka kwa Alikiba. Tarehe 25
Julai, 2014 Alikiba ameachia single mbili mpya kwa wakati mmoja ziitwazo
“Mwana” na “Kimasomaso”. Alikiba anajulikana ndani na nje ya Tanzania
kwa hit zake kama Cinderella, Mapenzi yanarun dunia, Single boy, na
Dushelele. Cinderela ndiyo wimbo ambao mpaka sasa umeweka rekodi ya
kuuza copy nyingi katika Afrika Mashariki mwaka 2008.
Mwaka
2012 Alikiba alishinda tuzo ya best Rhumba/ Zouk na wimbo wake wa
“Dushelele” katika tuzo za Kilimanjaro Tanzania Music Awards. Alikiba
anajulikana kwa uwezo wake mkubwa wa kuimba na utunzi wa nyimbo pamoja
na kuwa mburudishaji mkali sana katika show zake za live na mpaka sasa
ametembea nchi nyingi sana duniani kuburudisha wapenzi wa muziki. Sasa
unaweza kupata nyimbo mbili mpya za Alikiba bure katika tovuti ya www.mkito.com
Subscribe to:
Post Comments
(
Atom
)
0 comments:
Post a Comment